logo



ELIMU
Hadith in Swahili

h /p

620/258 kuwa mtaalamu au unasomea (elimu) au msikilizaji (wa elimu) na wala usiwe mjinga

621/259 atakaenyoosha njia kuomba (kutafuta) ndani yaka ilimu (basi) humrahisishia mwenyezi mungu njia ya (kwenda) peponi.

623/~ kila kitu kina nguzo, na nguzo ya hii dini ni uwanachuoni (utaalamu).

626/260 ombeni (jifunzeni) ilimu (hata) laukuwa katika china, kwani ilimu ni lazima juu yaa kila muislamu mwanamme na mwanamke.

631/261 na kwa hakika malaika wanaweka mbawa zao kwa anaejifunza ilimu kuwa radhi kwa ayafanyayo.

635/262 hakika mwenyezi mungu na malaika wake, na waliomo katika mbingu na ardhi, hata sisimizi(mdudu chungu) katika shimo lake, na hata samaki, wanamsalia juu ya mwalimu (anayefundisha) watu kheri.

636/263 atakae ita(watu)katika uongozi(kheri)basi anakuwa (anapata)ujira (thawabu)kama ujira wa watakaomfata,haupunguki katika ujira wao kitu.

673/279 akimpenda mmoja mmoja wenu ndugu yake basi amueleze(kuwa anampenda).

676/280 kuipenda dunia(basi)ni kichwa(sababu)cha kila kosa. Mlango wa kutazamana jamaa (ukoo)

693/287 ujamaa(wakuhusiana)unaninginia kwenye arshi unasema:atakaenifikia(nitazama,basi)atamfikia(atatazamwa na) mwenyezi mungu,na atakenikata(asienitazama,basi)atakatwa na mwenyezi mungu.

695/288 sadaka kwa masikini(thawabu yake)ni sadaka moja, na(sadaka)kwa jamaa (yako)inakuwa(thawabu)mbili sadaka na kumtazama.

696/288 haingii peponi mkataji (asietazama) jamaa (zake).

-- thawabu)kama ujira wa watakaomfata,haupunguki katika ujira wenu



next page

 

 

vs.3.1


home

latest update: Sat, 10 Jul 2010

2000-10-09





* living Islam – Islamic Tradition *
https://www.livingislam.org